Image
Image

Kituo kimoja cha redio na mashirika mawili ya magazeti yapigwa yazuiwa kuendesha shughuli zao Sudan Kusini.


Vikosi vya usalama vya Sudan Kusini vimepiga marufuku kituo kimoja cha redio na mashirika mawili ya magazeti kuendesha shughuli zao za kazi.

Miongoni mwa mashirika hayo ya habari yaliyowekewa marufuku ni gazeti la Al-Rai la lugha ya Kiarabu, The Citizen la Kiingereza pamoja na kituo cha redio cha sauti ya uhuru kinachorusha matangazo katika mji mkuu wa Juba nchini Sudan Kusini.

Ingawa vikosi vya usalama vimezuia mashirika hayo kuendesha shughuli zao, serikali ya Sudan Kusini bado haijatoa maelezo rasmi kuhusiana na ilani ya marufuku.

Kwa upande mwingine, mashirika hayo yanadaiwa kupigwa marufuku kutokana na sababu za kiusalama nchini humo.

Kamati ya Umoja wa Ulaya iliyoko Sudan Kusini imeripotiwa kutoa tahadhari kwa serikali ya nchi kutokana na suala hilo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment