RAIS Jakaya Kikwete amesema kuwa kiongozi anapokuwa amemaliza muda
wake wa uongozi na kustaafu, hawezi tena kuanza kudai kwa nini
hasikilizwi na uongozi mpya na kwa nini kuomba ushauri.
Rais Kikwete aliyasema hayo usiku wa kuamkia Jumatano alipozungumza
katika hafla ya kumuaga ambayo iliandaliwa na Majeshi ya Ulinzi na
Usalama ya Tanzania kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, mjini Dar es
Salaam.
“Nilisikia mtu mmoja analalamika majuzi kuwa anahama chama kimoja
kwenda kingine kwa sababu haombwi ushauri. Sasa wewe ulikwishakuwa
Waziri Mkuu, umemaliza ngwe yako ya uongozi, unalazimisha kuombwa
ushauri kwa nini?” Alieleza Rais Kikwete.
Aliongeza: “Mimi namaliza ngwe yangu ya uongozi. Nastaafu. Naondoka.
Kama Rais anayekuja ataona ni jambo mwafaka kutaka ushauri, nitachangia
kwa kadri ya uwezo wangu. Lakini kiongozi aliyestaafu hawezi kulazimisha
kuombwa ushauri.
“Rais yeyote anakuwa amekamilika. Anao washauri wake. Kama ni kuhusu
usalama mpo nyie wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama ambavyo
vimekamilika. Mtampa ushauri Rais anayekuja kama mlivyokuwa mnanipa
mie.”
Aidha, aliwaambia maofisa hao wa vyombo vya ulinzi na usalama: “Na
wala siombi nyie mje kwangu kuomba ushauri kwangu. Nendeni kwa Rais na
Amiri Jeshi Mkuu wetu. Vinginevyo mtanitengenezea fitina na kiongozi
wangu.
Sitalazimisha wala kulalamika kuwa sijaombwa ushauri.” Rais Kikwete
anamaliza muhula wake wa pili kikatiba baadaye mwaka huu kumpisha Rais
wa Awamu ya Tano.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment