Image
Image

Afya ya mama na mtoto kuimarika baada ya kupatiwa kipimo cha ULTRASOUND.


Shirika la kimataifa linalolenga kusaidia afya ya mama na mtoto lenye makao makuu yake nchini Australia (IHAN) limesaidia mashine mbili za kisasa zinazojulika kwa jina la ''ULTRASOUND''ili kupunguza adha wanayokabiliana nayo akina mama wajawazito ya kukosa huduma hiyo na kusababisha vifo vinavyoweza kuzuilika. 
Akizungumza jijini Tanga wakati wa makabidhiano ya mashine hizo ndogo zenye uwezo mkubwa kiutendaji,mjumbe wa shirika hilo Bibi,Zahra Nuru amesema lengo ni kusaidia hospitali ya rufaa ya mkoa wa Tanga ya Bombo na ile ya wilaya ya Pangani ambapo wahisani wameelekeza kuwa akina mama wajawazito wanapofika kwa ajili ya huduma hiyo wasitozwe fedha na kila baada ya miezi sita wapewe taarifa zinazoonesha imesaidia akina mama wangapi na walionusurika kifo baada ya kupta huduma ya mshine hizo.

Amesema hatua hiyo inafuatia makundi ya akina mama kutokuwa na uwezo wa kulipia huduma hiyo na hivyo kusababisha kati ya kina mama 100,000 wanaobeba ujauzito kila mwaka kati yao 400 hufariki dunia kwa sababu ya matatizo mbali mbali ya ujauzito na wakati wa kujifungua.

Kabla ya kukabidhiwa mashine hizo,katibu tawala mkoa wa Tanga Bwana.Salum Chima ameshukuru kwa msaada huo na kuwaagiza watendaji wa hospitali husika kuhakikisha wanapata wataalam wenye uzoefu na matumizi yake ili kuepuka matumizi mabaya yasiyoweza kupunguza au kumaliza kabisa tatizo la huduma zinazotolewa na mashine hizo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment