Image
Image

Kituo cha kulelea watoto wanaoishi mazingira magumu chavamiwa na vibaka.


Kituo kinacholea watoto waliotoka katika mazingira hatarishi cha imani kilichhoko mjini Shinyanga kinakabiliwa na changamoto kubwa ya kuvamiwa na vibaka nyakati za usiku na kupora mali za kituo hali inayosababishwa na ukosefu wa uzio ambapo pia hali hiyo inatishia usalama wa watoto wa kike kufanyiwa vitendo visivyofaa.
Meneja msaidizi wa kituo bw.saidi sakala amedai tangu kituo kianzishwe mwaka (1993) hakijawahi kuwa na uzio jambo ambalo limekua ni kikwazo kwao kutokana na vibaka wanaoingia mchana na usiku kupora mali za kituo na hivi sasa wanapora hata nguo na viatu vya watoto na kutishia kuwadhuru watoto wa jinsia ya kike.

Naye meneja wa NSSF mkoa wa Shinyanga Bw.James Mashinga amesema NSSF kama shirika la hifadhi ya jamii lina wajibu wa kuhakikisha makundi ya watu wenye uhitaji kama watoto wa kituo cha imani wanasaidiwa ili kuboresha maisha yao huku akitoa mwito kwa mashirika mengine ya binafsi na ya serikali kujenga utamaduni wa kusaidia makundi hayo ili kuondoa hali ya unyonge na kujisikia kama binadamu wengine.

Nao baadhi ya watoto wanaishi katika kituo hicho wamewataka wasamaria wema yakiwemomashirika ya serikali na binafsi kuwasaidia kwa kutoa misaada ya chakula na mahitaji mengine kama shirika la NSSF linavyofanya mara kwa mara hali itakayoondoa adha na wasiwasi wanayopata kutokana na mazingira ya kituo chao.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment