Kocha wa zamani wa timu ya soka ya Uganda akabiliwa na kesi ya ulawiti.
Chris Mubiru,aliyewahi kuhudumu kama kocha wa timu ya soka ya Uganda, amefunguliwa mashtaka na mahakama kwa madai ya ulawiti.
Mahakama ya mji wa Kampala ilimpata na Mubiru kuwa na hatia kufuatia maelezo na ushahidi uliotolewa na mashahidi watano.
Kwa mujibu wa sheria za Uganda, ulawiti ni kitendo cha uhalifu ambacho hukumu yake huwa ni kifungo cha miaka hadi 18 gerezani.
Jaji mkuu wa mahakama Flavia Nabakooza amearifu kusikizwa tena kwa kesi ya Mubiru tarehe 18 Septemba ambapo hukumu itatolewa.
Nchi ya Uganda ilipitisha sheria ya kupinga mahusiano ya jinsia moja na kuweka hukumu ya kifungo cha maisha kwa wahusika.


0 comments:
Post a Comment