Image
Image

Majambazi wakiwa na silaha za jadi wameteka magari ya mizigo na magari madogo kisha kujeruhi Mtwara.

Kundi kubwa la watu wanaodaiwa kuwa ni majambazi wakiwa na silaha za jadi,wameteka magari ya mizigo  na magari madogo binafsi,kujeruhi vibaya watu waliyokuwemo kwenye  magari hayo na kuwapora fedha, simu na vitu vingine.
Tukio  hilo limetokea  majira ya saa sita usiku wa kuamkia leo katika Mji wa Ndanda  Mkoani Mtwara ambapo watu hao  waliweka kizuwizi cha magogo kati kati ya barabara ya Masasi -Lindi  na kuzuia magari yote yaliyopita katika eneo hilo.
Mashuhuda walionusurika katika  tukio hilo wamedai muda mfupi baada ya tukio walitoa taarifa Kituo cha Polisi Ndanda,Polisi Wilaya ya Masasi na  Polisi Mkoa wa Mtwara lakini hawakufika katika tukio kwa muda muafaka japo majambazi hao walichukua zaidi ya saa moja na nusu wakiendelea na kitendo  cha uporaji.
Dakika chache kabla ya Askari Polisi kufika katika eneo la tukio watu hao walitoweka na kusikika wakitamka tuondoke noma inakuja.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment