Image
Image

MKAPA awataka viongozi wajao wa awamu ya tano kuhakikisha uhusiasiano kati ya Tanzania na nchi za Afrika unadumishwa.


Rais mstaafu wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania awamu ya tatu Mh.Benjamini Willium Mkapa amewataka viongozi wajao wa awamu ya tano kuhakikisha uhusiasiano kati ya Tanzania na nchi za Afrika unadumishwa ili kuweza kuimarisha na kuendeleza soko la pamoja litakalosaidia kukuza na kuinua  uchumi wa watanzania.  

 akihutubia maelfu ya wananchi mjini bukoba Mheshimiwa Mkapa amesema ili uchumi wa watanzania uimarike ni lazima mahusiano ya nchi hii na nchi jirani yaboreshwe pamoja na kuweka ulinzi katika  mipaka ya kimataifa  ili kuhakikisha kusiwepo machafuko yanayoweza kuhatarisha usalama wa raia na mali zao.

Kwa upande wake mwenyekiti wa chama cha mapinduzi mkoa wa Kagera Costansia Buhiye amewataka wananchi kukumbuka historia ya nchi hii ilikotoka na inakokwenda huku akiwataka kutowaunga mkono  viongozi wanaodandia vyama vya siasa kwa uchu wa madaka na kuwaomba wananchi kuchagua viongozi kutoka ndani ya chama cha mapinduzi kwakuwa wao ndio wanauwezo wakusimamia shughuli za maendeleo ya wananchi na kuhakikisha taifa linapiga hatua zaidi kiuchumi.

nao baadhi ya wagombea wanafasi za ubukonge katika mkoa huo wamewaomba wananchi kuwachagua ili waweze kushirikina na mgombea urais kwa tiketi ya chama hicho John Pombe Magufuri katika kusuma gurudumu la maendeleo ya wananchi wa  mkoa huo na taifa kwa ujumla.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment