Image
Image

News Alert:Rais wa Guetemala Otto Perez Molina amejiuzulu.


Rais wa Guetemala Otto Perez Molina amejiuzulu nafasi hiyo kufuatia kutakiwa kufanya hivyo na sasa taasisi za usalama nchini humo zimeamriwa kumkamata na kumfikisha mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.
Molina amejiuzulu ikiwa imepita saa chache tangu bunge la nchi hiyo kumuondolea kinga ya kutoshtakiwa na sasa atakabiliana na  madai ya rushwa yanayomuandama ya ubadhirifu wa mamilioni ya dola za huduma za forodha.

Jaji aliyeamuru molina akamatwe amesema amefanya hivyo kwa kuzingatia katiba ya nchi hiyo ambapo pia ameagiza katika kipindi ambacho vyombo vya ulinzi nchini humo vikifanya mchakato wa kumkamata haruhusiwi kutoka nje ya nchi hiyo.

Tayari  molina   ambaye muhula wake wa uongozi ulikuwa ukimalizika mwezi januari mwakani amesema atatii mambo yote atakayoambiwa afanye na vyombo vya sheria katika nchi hiyo ya Hungary ambapo kujiuzulu kwake pia kulichangiwa na maandamano ya wakazi wa nchi hiyo waliokuwa wakimpinga.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment