Meneja wa kampeni wa vyama
vinavyounda umoja wa katiba(UKAWA) na waziri mkuu mstaafu wa serikali ya CCM ya
awamu ya tatu BW FREDERICK TLUWAY SUMAYE amewataka watanzania kupuuza tuhuma za
ufisadi zilizotolewa na aliyekuwa katibu mkuu wa CHADEMA Dr.Wilborad Slaa dhidi
ya mgombea urais wa UKAWA Bw. Edward Lowassa pamoja na yeye na kueleza kwamba
hawatapoteza muda wa kumjibu kwani hizo ni hila zilizopangwa kutaka kufifisha
mabadiliko wanayohitaji kwa watanzania
Bw.Sumaye ametoa kauli hizo saa
chache baada ya kuwasili kwenye uwanja mdogo wa ndege wa Haydom na kuzindua kampeni
ya ubunge kwa jimbo la Hanang mkoani Manyara kwa kuwanadi wagombea udiwani na
ubunge wa UKAWA kabla ya kuanza kutembelea ngome za CCM,huku akiwataka wananchi
kumuunga mkono mgombea wa urais wa ukawa na wagombea viti vya ubunge na udiwani
wa ukawa ili kuunda serikali imara itakayowaletea mabadiliko wananchi katika
huduma za jamii.
Hata hivyo bw sumaye akimnadi
mgombea ubunge wa chadema Bw. Magoma Derick Magoma na madiwani wake Bw.Sumaye amewataka wapigakura
kuwachagua wagombea hao ambao watapambana na kero za rushwa,maji ,barabara
vijijini na elimu hasa kuondokana na wanafunzi kukaa juu ya mawe ambazo
hazijatatuliwa kwa miaka 10,mgombea ubunge huyo akiahidi kurejesha mashamba ya
shirika la taifa la chakula kwa wananchi.
This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.
0 comments:
Post a Comment