Image
Image

Polisi wapiga marufuku vikundi vya ulinzi vinavyomilikiwa na vyama vya siasa Nchini.


Polisi Mkoani  Dodoma imepiga marufuku shughuli za vikundi vya ulinzi vyenye mwelekeo wa kijeshi vinavyomilikiwa na vyama vya siasa na kuonya kuwa haitakuwa na mzaha kwa mtu, kikundi au taasisi itakayokiuka katiba katika kipindi cha hiki cha kampeni na baada ya uchaguzi mkuu.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma  DAVID MISIME pia amevitaka vyama vya siasa, wafuasi wao na wananchi wa mkoa huo, kuzingatia utii wa sheria katika kipindi chote cha kampeni na baada ya kupiga kura na kutangazwa matokeo na kisha kuapishwa kwa waliochaguliwa.
Katika hatua nyingine, jeshi hilo kwa kushirikiana na Mfuko wa Pensheni wa Serikali - LAPF-  limemkamata mtu aliyetambuliwa kwa jina la DAVID MAGESA MAKALI na kumfikisha mahakamani,  baada ya kujifanya mtumishi wa TAMISEMI na mifuko ya  LAPF, PSPF na ofisi ya Katibu Mkuu Wizara ya Afya, kwa kuwatapeli wastaafu Mamilioni ya Shilingi katika mikoa 15 nchini huku akijifanya kuwa yeye ni ofisa wa taasisi hizo anaye shughulikia pensheni.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment