Image
Image

JK:Tutafunga kamera za CCTV kuimarisha ulinzi wakati wa Uchaguzi Mkuu.

Kampeni za uchaguzi mkuu wa mwezi Oktoba mwaka huu nchini Tanzania zimepamba moto huku kila mgombea akitoa ahadi kubwa na nyingi kwa wapiga kura.
Uchaguzi wa mwaka huu nchini Tanzania unatarajiwa kuwa na hali ya kipekee katika kila upande na serikali ya nchi hiyo imesema imejiandaa vilivyo kulinda usalama.
Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania amesema kuwa atafunga kamera maalumu za CCTV katika miji mikuu ya nchi hiyo kukabiliana na wahalifu nchini humo.
Rais Kikwete amesema katika hafla ya kuagana na wapiganaji na walinzi wa usalama wa Tanzania iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Diamond Jubilee, jijini Dar es Salaam kuwa, Serikali yake inakamilisha mpango wa kufunga kamera hizo ili kuimarisha ulinzi na usalama wa raia.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment