Image
Image

Shirika la Hisani la Madaktari Wasiokuwa na Mipaka limetaka kuzuia kuenea kwa ugonjwa wa Surua.

Shirika la Hisani la Madaktari Wasiokuwa na Mipaka limetaka kuzuia kuenea kwa ugonjwa  wa Surua katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambao umeua watu 320 na kuambukiza wengine Elfu-30.
Mratibu wa shirika hilokatika Jamhuri ya Kidemokrasi ya  Kongo, Dakta  MICHEL JANSSENS ameonya kuwa janga la afya litaikumba nchi hiyo iwapo ugonjwa huo unaoenea kwa kasi  katika jimbo la Katanga hautazuiliwa ndani ya siku 60 zijazo.
Amesema hatua ya haraka inahitajiwa kuchukuliwa sasa kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa huo kwani itakuwa vigumu kuwafikia wagonjwa wakati wa msimu wa mvua unaotarajia kuanza ndani ya miezi miwili.
Mwezi uliopita Umoja wa Mataifa ulitoa Dola Milioni 2 na Laki-4 kusaidia serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya  Kongo na makundi mengine ya kibinadamu kusaidia kukabiliana na mlipuko huo.
Lakini shirika hilo linasema fedha peke yake haitoshi bali watendaji zaidi kwenye uwanja wa mapambano ambapo hadi sasa ni shirika hilo pekee linalotibu na kuchanja watoto.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment