Mgombea mwenza wa urais kwa tiketi
ya chama cha Demokrsia na maendeleo ( CHADEMA ), anayewakilisha vyama vinne
washirika vya umoja wa katiba ya wananchi ( UKAWA ) Mh. Juma Duni Haji
amewataka watanzania kumnyima kura mgombea wa chama cha mapinduzi ( CCM ),
Dk.John Pombe Magufuli kutokana na kuvunja nyumba za wananchi maskini,kauli za
kejeli kwa wananchi wa kigamboni na kuhusika na uuzaji holela wa nyumba za
serikali kwa bei ya kutupa.
Mh.Duni Juma Haji ametoa mwito huo
kwa watanzania katika nyakati tofauti wakati akihutubia mikutano ya kampeni za
uchaguzi mkuu kwa wananchi wa wilaya za Rufiji, Mkuranga na Kisarawe mkoani Pwani
na kuongeza kuwa anazidi kushangazwa na kauli ya hivi karibuni ambayo mgombea
urais huyo wa CCM DK. JOHN POMBE MAGUFULI ameitoa akiwa mkoani Mtwara ya
kuwataka askari polisi kuwaua majambazi huku akihoji ni vipi serikali ya CCM
chini ya rais Jakaya Kikwete imeshindwa kupambana na wezi wa fedha za Umma.
Aliyewahi kuwa mwenyekiti wa chama
cha mapinduzi mkoa wa Dar es Salaam ambaye kwa sasa ni kada wa Chadema John Guninita
naye akapanda jukwaani kumzungumzia mgombea urais wa chama cha mapinduzi
dk.John Pombe Magufuli.
Aidha mgombea mwenza huyo wa urais
kupitia ukawa,akihutubia mkutano wa kampeni za uchaguzi mkuu katika jimbo la Kisarawe
uliofanyika kwenye uwanja wa shule ya msingi Chanzige,Mh.Juma duni Haji
amewaomba wananchi kumchagua mgombea ubunge wa jimbo hilo anayetokana na chama
cha wananchi CUF Rashid Mwinshehe Mzange, maarufu kama Kingwendu kwa jina la
usanii na alipopandishwa jukwaani ili kuomba kura.





0 comments:
Post a Comment