Umoja wa Mataifa umesema dunia ilikuwa inawaangusha wakimbizi wa Syria zaidi ya Milioni nne wengi wao wakiwa wamekimbilia nchi jirani za Mashariki ya Kati.
Uchunguzi wa uliofanywa na Umoja huo umekosoa kushindwa kwa dunia kuwalinda wakimbizi wa nchi hiyo na kusema kushindwa huko kumechochea mgogoro wa sasa wa wahamiaji Barani Ulaya.
Ripoti ya hivi karibuni ya uchunguzi huo inasema Wasiriya 2,000 waliokuwa wanajaribu kwenda Ulaya wamekufa maji katika Bahari ya Kati au Mediterranean.
Zaidi ya wakimbizi Milioni nne wa Syria wako Uturuki, Lebanon, Jordan, Iraq, Misri na Kaskazini mwa Afrika.
Home
Kimataifa
Uchunguzi uliofanywa na Umoja wa Mataifa wakosoa kushindwa kwa dunia kuwalinda wakimbizi.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)





0 comments:
Post a Comment