Zaidi ya asilimia 70 ya wakazi wa wilaya ya Kyela wanapata huduma za afya hususan matibabu katika Hospitali za wilaya za jirani hali inayosababishwa na serikali kutowekeza vya kutosha katika Hospitali za umma wilayani humo.
Akizungumza kwenye
mkutano wa hadhara ambao umeandaliwa maalum kwa ajili ya uzinduzi wa kampeni za
uchaguzi wa ubunge na madiwani kupitia chama cha Demokrasia na maendeleo
wilayani Kyela,mgombea ubunge wa jimbo la Kyela,Abrahamu Mwanyamaki amesema
wilaya ya Kyela inakabiliwa na changamoto kubwa ya ubovu wa miundombinu ya
afya,jambo ambalo linasababisha zaidi ya asilimia 70 ya wananchi wilayani humo
kupata huduma za afya katika wilaya za jirani.
Mbunge wa mbeya mjini
aliyemaliza muda wake,Joseph Mbilinyi maarufu kwa jina la Mr.ii Sugu amesema
kutokana na huduma mbovu za Kiafya zinazotolewa na serikali ya chama cha
mapinduzi, wananchi wanahitaji mabadiliko ambayo kwa mkoa wa mbeya wenye
majimbo 13 ya uchaguzi UKAWA wanauhakika kunyakua majimbo zaidi ya 10.
Baadhi ya viongozi wa
chama cha Demokrasia na maendeleo wamewataka mahasimu wao kisiasa,kuendesha
kampeni za kistaarabu ili kutoa fursa ya wananchi kuisikiliza sera, huku
wakidai kuwa wanaimani kubwa na wagombea wao.


0 comments:
Post a Comment