Mgombea mwenza wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo - CHADEMA , JUMA DUNI HAJJI, amewaahaidi wakazi wa majimbo ya Isimani na Kalenga kwamba wakiingia madarakani watarejeshewa mashamba yao yaliyobinafsishwa kwa wawekezaji na wamesshindwa kuyaendeleza.
Katika mikutano ya kampeni mgombea mwenza huyo ameendelea kunadi sera za chama hicho na kumuombea kura mgombea wake wa Urais EDWARD LOWASSA kwa wananchi wa Mkoa wa Iringa.
Akihutubia mikutano ya kampeni za uchaguzi mkuu katika majimbo ya Isimani na Kalenga JUMA DUNI HAJJI amesema iwapo Watanzania watamchagua LOWASSA, atahakikisha wakulima na wafugaji wanaingizwa katika mpango wa matumizi bora ya ardhi ili kukomesha migogoro pamoja na kuwajengea mazingira mazuri wafanyabiashara ndogondogo kwa kuwaondolea utitiri wa kodi ambazo zinadaiwa kuwanufaisha baadhi ya watu wachache.
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Isimani kupitia CHADEMA PATRICK ole SOSOPI amesema akichaguliwa kuwa mbunge wa jimbo hilo atahakikisha maisha ya wananchi wanaoishi jirani na Hifadhi ya taifa ya Ruaha yanakuwa ya amani na furaha.
Home
News
Wakazi wa majimbo ya Isimani na Kalenga kurejeshewa mashamba yao yaliyobinafsishwa kwa wawekezaji - CHADEMA.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)


0 comments:
Post a Comment