Image
Image

Watanzania wametakiwa kutoaamini kauli za vyama vya upinzani,kuwa Chama cha Mapinduzi hakijafanya lolote.

Watanzania wametakiwa kutoaamini kauli za vyama vya upinzani,kuwa Chama cha Mapinduzi hakijafanya lolote kwani  imeboresha huduma za jamii kama elimu, afya, miundombinu, kilimo na huduma kwa makundi maalumu ya vijana, wazee na walemavu kwa asilimia 88.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa CCM Mkoani Lindi,  AMIRI MKALIPA amesema hayo kwenye  uzinduzi wa kampeni ya CCM, Kata ya Mipingo Wilaya ya Lindi Vijijini uliotumika kumnadi mgombea wa udiwani wa kata hiyo.
MKALIPA amesema katika kipindi cha miaka 10 cha utekelezaji wa ilani CCM imejenga shule za sekondari 4,576 sawa na ongezeko la asilimia 162, waalimu waliohitimu Elfu-73 na 407, wakati ujenzi wa barabara za lami imefikia Kilometa Elfu 17.6.
Amewataka  Watanzania kukipigia kura Chama cha Mapinduzi  kwenye uchaguzi mkuu ujao, ili kulinda na kuendeleza mafanikio yaliyopatikana.
Kwenye uzinduzi huo wanachama 10 wa Chama cha Wananchi - CUF akiwemo katibu wa chama hiho  wa Kata ya Mipingo wamejitoa chama hicho na kujiunga na Chama cha Mapinduzi.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment