Katibu wa chama hicho, mkoani humo, Mhandisi
Mohamed Ngulangwa, aliyasema hayo katika taarifa yake kwa vyombo vya habari na
kuongeza kuwa, wamemuandikia barua Mkuu wa Mkoa huo, Said Meck Sadiki ili
kumuomba ayapokee maandamano hayo ya amani.
"Tumepanga kufanya maandamano hayo Desemba 16
mwaka huu, tukianzia katika ofisi zetu za Mkoa eneo la Keko Maduka Mawili
na kuishia Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Ilala Boma," alisema.
Alisema lengo lingine la kufanya maandamano hayo ni
kumtaka Rais asimamie uongozi bora wenye lengo la kuirudisha nchi kwenye
misingi iliyoasisiwa na wazee Hayati Mwalimu Julius Nyerere na Mzee Abeid Aman
Karume.
Aliongeza kuwa, ilani ya chama chao ukurasa wa saba
inaelezea ndoto ya ACT-Wazalendo ni kuona Taifa linajitegemea kiuchumi,
kiutamaduni, kudumisha usawa, ustawi wa jamii, uwajibikaji, demokrasia, uongozi
bora.
Mhandisi Ngulangwa alisema chama hicho kinaamini kuwa,
mambo hayo yatatekelezwa vizuri kama nchi itajiwekea miiko ya uongozi kama
inavyoelezwa na Azimio la Tabora lililohuishwa kutoka Azimio la Arusha.
"Lengo lingine ni kumuomba Rais ahakikishe nchi
kupitia mamlaka husika, inasimamia mfumo wa matumizi ya fedha kama inavyosema
katika ilani ya chama chetu ukurasa wa 23.
"Hata hivyo, yote hayatakuwa na maana
kama mfumo wa fedha kupitia benki utakuwa umeshikwa na wageni kwani nchi
yetu haiwezi kuendelea ikiwa benki kubwa zitakuwa zimebinafsishwa,"
alisema.
Alisema uanzishaji benki uliofanyika mwaka 1967 na
kuundwa kwa Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Benki ya Nyumba na Benki ya
Maendeleo Vijijini ni maamuzi ya msingi kwa maendeleo ya nchi.
0 comments:
Post a Comment