Image
Image

SAMIA azitaka taasisi za umma kuanzisha kampeni maalum kukuza maadili nchini.

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amezitaka taasisi mbalimbali za umma na za kiraia kuanzisha kampeni maalum ya kukuza maadili nchini. 
Amesema hayo kwenye maadhumisho ya nane ya kitaifa ya Haki za Binaadamu yaliyofanyika leo jijini Dar es Salaam na kuongeza kuwa  maadili ni chanzo cha huchochea utu na haki za binaadamu.
Amesema kuwa, kulinda na kuheshimu haki za binaadamu ni wajibu wa kila mtu katika jamii ambapo serikali, familia au kaya na mtu mmoja mmoja kuhusika kuzilinda.
Amesema Serikali ya Awamu ya Nne imepokea kiporo cha Katiba na kwamba serikali yake itaheshimu maoni ya wananchi yaliyokusanywa na kuhakisha kuwa, yanazingatua haki za binaadamu.
Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora, Bahame Nyanduga amesema kuwa haki za binaadamu zimeimarika nchini licha ya changamoto za mauaji yanayotokana na imani za kishirikina pamoja na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino), wazee, ukatili dhidi ya watoto na jinsia, mauaji ya kujichukulia sheria mkononi na uwelewa mdogo wa haki za binaadamu.
Maadhimisho ya mwaka huu ni ya nane tangu yalipopitishwa na kuadhimishwa mwaka 2008 ambapo Tanzania inaungana na mataifa mengine katika kuadhimisha siku hiyo na kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni ‘Haki zetu, Uhuru wetu Daima’
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment