Diwani mteule wa Ubungo, Boniface Jacob (Chadema
(kushoto),aki[pongezwa baada ya kuteuliwa na na chama hicho kugombea umeya wa
Manispaa ya Kinondoni hivi karibuni.
Miongoni mwa vyama vinavyounda Ukawa kwenye uchaguzi
huo ni Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na Chama cha Wananchi (CUF).
Katika Manispaa ya Kinondoni Ukawa wana jumla ya madiwani pamoja na wabunge 38
huku CCM ikiwa na 27.
Zomeazomea, kelele na kejeli ziliibuka kwenye
uchaguzi huo uliopangwa kufanyika kwenye ukumbi wa manispaa hiyo kabla ya zoezi
la uapishaji wa madiwani na uchaguzi wa meya kufanyika.
Ukawa ndio walioanzisha kelele hizo wakitaka
madiwani ambao wanatoka nje ya Dar es Salaam waondoke na kuwapisha madiwani wa
Dar es Salaam pekee jambo ambalo lilizua vurugu.
Katika shughuli hiyo ya uapishaji, Ukawa walieleza
kuwa baadhi ya madiwani na wabunge wa viti maalum kutoka Zanzibar ambao
waliletwa ili kuwa upande wa CCM kama madiwani kutoka Jimbo la Kinondoni.
Ukawa wameeleza kuwa, sheria na taratibu za uchaguzi
huo zinawanyima sifa ya kuwepo kwenye shughuli ya uchaguzu wa meya wa manispaa
hiyo.
Kutokana na hali hiyo, Ukawa walitaka kupata
ufafanuzi kutoka kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Mussa Natty ili kutoa
ufafanuzi juu ya hilo huku wakimtaka kuwatoa makada hao kutoka Zanzibar.
Malumbano hayo yaliyodumu kwa takribani nusu saa
bila kufikia muafaka na kusababisha baadhi ya wanachama kuingia ndani ya ukumbi
huo na kuleta vurugu.
Hali hiyo ilimlazimu Natty kughairisha shughuli hiyo
kwa muda na kutoka nje huku akisema, atarejea baada ya saa moja ili waweze
kupata muafaka.
Mkurugenzi huyo alirejea akiambatana na Mwanasheria
Mkuu wa Manispaa ya Kinondoni, Bunton Mahenge ambaye alighairisha shughuli
hiyo.
“Tumeghairisha shughuli hii kutokana na kutofikia
muafaka, hivyo tumeona tulipeleke suala hili mbele kwa maandishi ili kupata
ufafanuzi kama madiwani hawa kutoka Zanzibari wanatakiwa kuwepo au hawatakiwi.
Tumewaandikia tunasubiri majibu ya maandishi toka TAMISEMI kisha tutawajuza
siku ya kuja tena.”
Akizungumza na waandishi mara baada ya kutoka nje ya
ukumbi Mbunge wa Jimbo la Kibamba, John Mnyika amesema kuwa ujio wa wajumbe kutoka
Zanzibar ni mpango mkakati wa kikao cha Kamati kuu ya CCM kilichokaliwa juzi
Ikulu ili waje kuongeza idadi ya madiwani.
“Tumezigundua mbinu zao na hawatupati. Wamezoea
kuiba safari hii tupo macho, na mtindo huu wa kuwaongeza madiwani wa Zanzibar
umefanyika hata katika Wilaya ya Temeke na Ilala, wanataka tuseme ili waseme
tumeleta fujo kuvuruga uchaguzi sasa sisi hatutoki hadi kieleweke,” amesema
Mnyika.
Pia amesema, wamebaini mbinu za CCM na nia ya kuleta
madiwani hao katika kila wilaya kwa sababu CCM imepata idadi ndogo ya madiwani
katika Jijin la Dar es Salaam.
Anaeleza kuwa lengo la kuongezwa kwa madiwani hao ni
CCM kutaka kuongeza udadi ya kura ili wafanikiwe kutwaa nafasi ya Meya wa Jiji
la Dar es Salaam.
0 comments:
Post a Comment