Image
Image

Latest News:Upotevu Mwingine wa Makontena 2431 wanaswa na waziri mkuu Majaliwa.



Waziri mkuu Mhe.Kassimu Majaliwa kwa mara nyingine amefanya ziara ya kustukiza kwa mifumo ya uingizaji na utoaji mizigo bandarini na kubaini kotena za mizigo 2431 zinazomilikiwa na watu kumi tu zikiwa zimeingizwa na kutolewa bandarini bila ushuru na kulikopesha taifa mapato ya mabilioni ya shilingi.

Waziri mkuu Mhe.Kassimu Majaliwa aliyeingia kwa staili ya kuanzia vitengo vidogo vya kimfumo ya IT akihoji uwezekano wa mifumo hiyo kuzuia wizi na utoroshaji wa makontena huku akilishwa maneno matamu na viongozi wa bandari akiwemo meneja wa bandari Bw.Abel Muhanga kuwa kwa mifumo hiyo kuwa hakuna uwezekano wa mtu yoye kupitisha mzigo bila kulipa ushuru.

Hali hiyo ilibadilika mara baada ya waziri mkuu Kassimu Majaliwa kutoa ripoti ya ukaguzi wa Marchi hadi Desemba Mwaka jana kuwa kontena 2532 zimethibitishwa na wakaguzi kuwa zimepitishwa bila kulipa ushuru na konyeshwa majina ya wahusika hali ilioyoonekana kuwa shubiri kwa meneja wa bandari akikiri kuwatambua na kujitetea kuwa angeambiwa baadae.

Katika hali hiyo Mhe.Majaliwa amemuagiza meneja wa bandari kuwa hadi jioni ya leo awe amewasilisha majina yote ya wakweepaji kodi wakubwa na hatua za kisheria zichukuiwe mara moja.

Aidha Mhe.Majaliwa alipita shiirika la reli TRL kukagua miradi ambapo amesikika akitoa kauli ya kuwashutumu kutumia zaidi ya shilingi bilioni 200 isivyo tarajiwa.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment