Image
Image

Maafisa TRA wabaini kuwa makonteina 9 yaliokuwa yamekatwa mbezi yamelipiwa kodi.

Maafisa wa  Mamlaka ya Mapato nchini waliofanya   ukaguzi wa awali katika makontena tisa yaliyokamatwa katika eneo la Mbezi Tanki Bovu Jijini Dar es Salaam wamebaini kuwa makonteina hayo yamelipiwa kodi na yametoka bandartini kwa kufuata utaratibu.
Makontena hayo yaliingizwa nchini kutoka China  yakiwa na vifaa vya ujenzi.
Wahusika wa kusafirisha makontena hayo kampuni ya  PMM ICD wamesema walilazimika  kupeleka   makontena  hayo  katika eneo hilo ili kuyahifadhi kabla ya kumfikishia mteja wao .
Mmiliki wa   makontena hayo  kampuni ya  Heritage Empire Co Ltd ,   mbali na kueleza kuwa  mali hiyo haina mashaka kwani  imeingizwa nchini na kuondolewa bandari ni  kwa kufuata taratibu zote ,  lakini alishikwa butwaa baada ya kuona makontena yake yamefikishwa katika eneo la Mbezi  badala ya   Bagamoyo  ambako mradi wa ujenzi ulipo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment