Image
Image

Mayunga aleza furaha yake baada ya kurekod na AKON.


MSHINDI wa 'Airtel Trace Music Stars’ Nalimi Mayunga amerudi nchini kutoka Marekani alipokwenda kwa ziara ya wiki moja kwa ajili ya kurekodi video yake na kupata mafunzo kutoka kwa mwanamuziki nguli Akon.

Nalimi Mayunga alisema hii imekuwa nafasi ya pekee maishani mwake na anapenda kuwashukuru sana Aitel na Trace kwa kumpatia fursa hiyo.

"Nimefurahia muda niliokaa Marekani na kupata wakati mzuri wa kumtembelea Akon nyumbani kwake na kurekodi video na kupata mafunzo ya muziki,” alisema.

Nalimi aliongeza kwa kusema fursa hiyo imempa mwanga zaidi katika namna ya kufikiri na kujipanga, ili kuzifikia ndoto zake katika tasnia ya muziki. 

"Nimejifunza mambo mengi sana kupitia mafunzo niliyopata kutoka kwa Akon ikiwemo jinsi ya kukabili jukwaaa, namna ya kuchezea sauti yangu, mafunzo ya sauti, namna ya kuandika na kutunga nyimbo na jinsi ya kuinua muziki wangu na kukuza kipaji changu kwa ujumla."

Nalimi aliyejawa furaha pia alieeleza shauku aliyonayo ya kutoa kibao hicho kwa kushirikiana na Akon na kusema kwamba kitafungua milangoyake katika ulimwengu wa muziki, kwani amepata nafasi ya kuingia na kurekodi wimbo wake kwenye studio ya Universal Hollywood yenye vifaa vya kisasa na vyenye teknologia ya juu.

"Nina uhakika video yangu itakuwa moja kati ya video bora za muziki sokoni na hivyo nawashurukuru sana mashabiki wangu, Watanzania kwa ujumla kwa kunipigia kura na kuniwezesha kufika hapa nilipo leo."

Akieleza zaidi kuhusu safari ya Mayunga, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Airtel, Beatrice Singano Malya alisema 'Tunafurahi kuwa sehemu ya kubadilisha maisha ya vijana wengi akiwemo Nalimi Mayunga. Tunaamini Mayunga atakuwa ni mfano utakaowavutia vijana wengi kuzifikia ndoto zao. Tunapenda kuwahamasisha vijana wengi zaidi kushiriki katika program zetu nyingi zenye lengo la kuwawezesha kufikia malengo yako kama vile Airtel Fursa, Airtel Rising Stars, Airtel Trace Music Stars na nyingine nyingi.”

Msimu wa pili wa shindano kubwa la muziki la Afrika la Airtel Trace Music Stars mwaka 2016 linategemea kuzinduliwa rasmi mwanzoni mwa Januari, mwakani na wanatoa wito kwa vijana wengi kushiriki pindi shindano hilo litakapotangazwa rasmi. 





Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment