WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amekutana na kufanya mazungumzo na
mabalozi watatu kutoka nchi za China, Jamhuri ya Sudan na Korea Kusini.
Akizungumza kwa nyakati tofauti na mabalozi hao ofisini
kwake Magogoni jijini Dar es Salaam, Waziri Mkuu aliwashukuru mabalozi
hao kwa pongezi walizokwenda kumpatia na kuahidi ushirikiano zaidi na
nchi zao.
Kwa upande wake, Balozi wa China, Dk Lu Youqing alisema Serikali
itaendelea kuisaidia Tanzania kwenye sekta za uendelezaji viwanda,
miundombinu, maji, afya na elimu, ikiwa ni ishara kuendeleza mahusiano
ambayo yamekuwepo kwa muda mrefu baina ya China na Tanzania.
Alisema Tanzania imeteuliwa kuwa miongoni mwa nchi tatu
zitakazosaidiwa na China kuendeleza viwanda na kwamba makubaliano ya
mpango huo yatafikiwa kwenye Mkutano wa Ushirikiano baina ya China na
Nchi za Afrika (FOCAC - 6) unaotarajiwa kuanza Desemba 4, mwaka huu
Johannesburg, Afrika Kusini.
Nchi nyingine mbili zitakazonufaika na mpango huo ni Kenya na
Ethiopia. Balozi wa Jamhuri ya Sudan, Dk Yassir Mohamed Ali alisema nchi
yake inao madaktari wengi na kwamba kumekuwa na majadiliano ya kuona ni
jinsi gani wanaweza kuja kuongeza nguvu kwenye sekta ya afya.
“Tuna madaktari wasiopungua 4,000 ambao wanahitimu kila mwaka na
tungependa kushirikiana na Tanzania katika eneo hili,” alisema Dk Ali.
Kwa upande wake, Balozi wa Korea Kusini, Chung Il ambaye pia alitumia
fursa hiyo kuagana na Waziri Mkuu Majaliwa, alisema anatumaini kuona
ubalozi wa Tanzania ukifunguliwa nchini mwao katika muda siyo mrefu.
Home
News
WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa ateta na mabalozi watatu kutoka nchi za China,Jamhuri ya Sudan na Korea Kusini.
Subscribe to:
Post Comments
(
Atom
)
0 comments:
Post a Comment