Image
Image

Majwega sasa huru kucheza Simba katika Ligi Kuu bara.

MCHEZAJI Brian Majwega raia wa Uganda sasa yupo huru kucheza Simba katika Ligi Kuu bara.
Kwa takriban wiki mbili sasa kumekuwa na mgogoro kati ya Simba na Azam FC kuhusu mchezaji huyo aliyesajiliwa na Azam mwanzoni mwa mwaka huu.
Mgogoro huo ulitokana na mchezaji huyo kufanya mazoezi Simba, jambo lililokuwa likipingwa na Azam kwa vile bado ilikuwa na mkataba naye. 
Akizungumza Dar es Salaam msemaji wa Simba, Haji Manara alisema wamefikia makubaliano maalumu na Azam na sasa Majwega ni mali yao.
“Majwega sasa rasmi Simba ni mchezaji wetu na tutamtumia kwenye ligi, tumefikia makubaliano maalumu na Azam jana jioni (juzi),” alisema Manara. Hata hivyo, si Simba wala Azam waliokuwa tayari kuzungumzia kwa kina aina ya makubaliano waliyoafikiana.
Kabla ya kurejea nchini Majwega alirudi kwao Uganda baada ya kuona hapati nafasi Azam, lakini pia alishindwa kucheza na kuamua kurudi nchini. Baada ya kurudi Majwega aliandika barua Simba akiomba kufanya mazoezi ili kulinda kiwango chake kwani hakuwa kwenye maelewano na klabu ya Azam.
Majwega alirejea nchini na kuomba kufanya mazoezi na Simba ili kulinda kiwango chake na ndipo Azam walipokuja juu kwamba hawatendewi haki na Simba. Hii si mara ya kwanza kwa klabu hizo, ambazo inaaminika ni marafiki kuingia kwenye mgogoro wa wachezaji.
Ilishawahi kuingia kwenye mgogoro wa kumgombea Shomari Kapombe na Ramadhani Singano, ambao kwa sasa wanacheza Azam FC.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment