Coutinho baada ya kurejea Dar es Salaam mwishoni mwa wiki
iliyopita, akitokea kwao Brazil kwa mapumziko mafupi, ambapo jana klabu hiyo
ilikuwa na kikao kujadili mustakabali wake ndani ya timu hiyo na kuamua
kuachana naye.
Habari zilizopatikana Dar es Salaam jana kutoka kwa mmoja wa
viongozi wa klabu hiyo, zinadai kuwa, kutokana na mchezaji huyo kutopata nafasi
kwa Kocha Mkuu wa timu hiyo, Hans de Pluijm, hawaoni sababu ya kuendelea na
mchezaji huyo.
Coutinho analipwa na klabu hiyo mshahara wa dola 3,000 za
Marekani kwa mwezi (zaidi ya sh.milioni 6 za Tanzania).
„Kama klabu inalipa kiasi chote hicho cha fedha kwa mwezi
kwa mchezaji huyo lakini hachezi, haina sababu ya kuendelea naye, tunajua ni
kipenzi cha mashabiki lakini hatuna jinsi kwa hilo,” kilidao chanzo hicho.
Pia kuna taarifa kwamba klabu kadhaa ikiwemo za St George ya
Ethiopia zinamtaka mchezaji huyo, hivyo Yanga ipo tayari kumuacha kwa sasa.
Lakini Yanga kwa sasa inafanya mchakato huo, kama pande
mbili zitashindwa kufikia mwafaka, basi raia huyo wa Brazil ataendelea kubaki
Yangahadimkatabawake utakapokwisha.
Coutinho alisajiliwa Yanga msimu uliopita chini ya kocha
Mbrazil mwenzake, Marcio Maximo na hadi sasa ameichezea klabu hiyo mechi 36 na
kuifungia mabao saba.
Alikuja nchini pamoja na mshambuliaji mwingine, Mbrazil
Genilson Santana Santos ëJajaí ambaye aliachwa baada ya nusu msimu akiwa
amecheza mechi 11 na kufunga mabao matano.
Wachezaji saba wa kigeni wanaokidhi kanuni ya Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania katika kikosi cha Yanga kwa sasa ni mabeki Mbuyu Twite (DRC),
Vincent Bossou (Togo), viungo Haruna Niyonzima (Rwanda), Thabani Kamusoko
(Zimbabwe), Coutinho (Brazil) na washambuliaji Amisi Tambwe (Burundi) na Donald
Ngoma (Zimbabwe).
0 comments:
Post a Comment