Image
Image

Newcastle yainyoosha Liverpool ligi kuu England.

Ligi kuu ya soka ya England iliendelea tena jana kwa mchezo mmoja pekee uliopigwa katika dimba la St James Park wenyeji Newcastle wakiwakaribisha majogoo wa London Liverpool, ambapo Newcastle walifanikiwa kuchomoza na ushindi mnono wa bao 2-0.
Dakika ya 69 ya mchezo katika harakati za kuokoa mpira uliopigwa na Georgino Winaldum, Martin Skrtel wa Liverpool alijikuta akijifunga katika harakati za kuokoa mpira huo.
Na dakika ya 93 ndani ya muda wa nyongeza Wina-Naldum aliamsha shangwe St James Park kwa kuandika bao la pili.
Kwa Ushindi huo sasa Newcastle wamekwea hadi nafasi ya 18 wakiwa na pointi 13 juu ya Sunderland na Aston Villa ambao wanaburuta mkia katika msimamo wa ligi.
Ligi hiyo inatarajiwa kuendelea tena leo Jumatatu kwa mchezo mmoja tu ambapo Everton watawaalika Crystal Palace.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment