Image
Image

Pluijm:Viwanja vingi vya soka nchini viko katika hali mbaya.

Viwanja vingi vya soka nchini viko katika hali mbaya kiasi cha kuhatarisha maisha ya wachezaji na hata watazamaji.
Kutokana na hali hiyo, kocha wa Yanga, Hans van der Pluijm, ameanza kusaka mbinu za kupata ushindi katika mechi zijazo za Ligi Kuu Tanzania zitakazochezwa kwenye Uwanja wa Mkwakwani jijini Tanga ambao mazingira yake amedai si mazuri.

Yanga itashuka kwenye uwanja huo kuikabili African Sport na Mgambo JKT Desemba 12 na 16.

Akizungumza,Pluijm alisema kikosi chake kinakuwa kwenye wakati mgumu kinapocheza nje ya Dar es Salaam, sababu kubwa ikiwa ni ubovu wa viwanja vya mikoani.

"Tunakuwa na wakati mgumu sana tunapocheza nje ya Dar es Salaam, timu pia hukamia," Pluijm alisema. 

"Tutacheza aina ya mpira utakaoendana na uwanja pamoja na wapinzani wetu, kikubwa tunataka ushindi bila kujali idadi ya magoli."

Kocha huyo alisema kuwa kutokana na changamoto hiyo, ameandaa programu maalum ya mazoezi itakayoendana na uwanja huo ili kupata matokeo mazuri katika mechi hizo mbili.

Katika mazoezi ya juzi na jana Pluijm, aliwasisitiza wachezaji wake kucheza mpira wa pasi ndefu huku akiwataka kutumia kila nafasi ya kufunga wanayoipata.

Katika hatua nyingine, wachezaji wa Yanga waliokuwa kwenye kikosi cha timu Kilimanjaro Stars na Zanzibar Heroes zilizong'olewa mapema kwenye michuano ya Kombe la Chalenji inayoendelea Ethiopia, wanatarajia kujiunga na wenzao Jumamosi kuendelea na mazoezi ya timu hiyo yanayofanyika kwenye Uwanja wa Boko Veteran.

Nyota wa Yanga walikokuwa kwenye vikosi hivyo ni Simon Msuva, Kelvin Yondani, Deus Kaseke, Salum Telela na Malim Busungu (Kilimnajaro Stars) pamoja na wale wa Zanzibar Heroes: Nadir Haroub 'Canavaro' na Haji Mwinyi.  

Kikosi hicho cha Yanga kitaondoka Dar es Salaam kwenda Tanga Desemba 7 tayari kwa michezo hiyo.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment