Image
Image

Simba,Yanga mguu sawa.

TIMU za Simba na Yanga zimetamba sasa zimeimarika baada ya wachezaji wao kurejea nchini wakitokea Ethiopia walikokuwa katika michuano ya Kombe la Chalenji. 
Wakizungumza kwa nyakati tofauti makocha wa timu hizo walisema wanaamini kuanzia leo wachezaji hao watakuwa wamejiunga na vikosi vyao na maandalizi yatakuwa yamekamilika.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Kocha Mkuu wa Yanga, Hans van der Pluijm, amesema wiki hii amepanga kubadilisha programu ya mazoezi kwa vile tayari atakuwa na wachezaji wake wote.
Kwa muda wa wiki tatu Yanga imekuwa ikifanya mazoezi kwenye uwanja wa Boko Veterani, huku ikitumia idadi kubwa ya wachezaji wa timu ya vijana, baada ya wale wa kikosi cha kwanza wengi wao kuwa Ethiopia katika michuano ya Chalenji.
“Nimefurahi kuona idadi kubwa ya wachezaji wangu wa kikosi cha kwanza tayari wamerudi kundini, mikakati yangu kuanzia sasa ni kubadili mpangilio wa mazoezi na kuongeza mkazo kuhakikisha timu inarudi kwenye kiwango chake, ili tuweze kupata matokeo mazuri kwenye mechi zetu za ligi,” alisema.
Alisema ana uhakika na wachezaji aliokuwa nao kwenye mazoezi na hata wale waliokuwa kwenye timu za taifa, lakini anachotaka kufanya ni kubaini utimamu wao ili kujua upungufu uliopo kabla ya mchezo wao wa mzunguko wa 10 wa Ligi Kuu dhidi ya Mgambo JKT ya Tanga mwishoni mwa wiki ijayo.
Wachezaji wa Yanga waliokuwa kwenye michuano ya Chalenji Ethiopia ni Ally Mustapha ‘Barthez’, Kelvin Yondan, Salum Telela, Deusi Kaseke, Simon Msuva na Malimi Busungu wote wa Tanzania Bara ‘Kili Stars’.
Wengine ambao walikuwa timu ya Taifa ya Zanzibar ni ‘Zanzibar Heroes’ ni Nadir Haroub ‘Cannavar’, Haji Mwinyi, Matheo Simon na Said Juma, ambapo pia alikuwpeo Amissi Tambwe aliyekuwa na timu ya taifa ya Burundi na Haruna Niyonzima wa Rwanda.
Kati ya wachezaji hao ni Niyonzima tu ambaye bado yupo Rwanda, ambapo timu yake ya Taifa leo inacheza mechi ya nusu fainali, wakati wachezaji wengine timu zao zimeshaondolewa na wamerejea nchini.
Kwa upande wake, Kocha Mkuu wa Simba, Dylan Kerr alisema anaamini kikosi chake sasa kitakuwa imara kujipanga kwa ajili ya mechi ya Ligi Kuu dhidi ya Azam Jumamosi wiki ijayo. Kerr, ambaye timu yake ipo kambini Zanzibar, alisema anaamini kutimia kwa kikosi chake kutampa fursa ya kuwapa mafunzo ya uhakika kwa ajili ya ligi hiyo.
Wachezaji wa Simba waliokuwa Kilimanjaro Stars ni Hassan Kessy, Jonas Mkude, Said Ndemla, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, wakati kwa Zanzibar Heroes ni Awadh Juma na Samir Haji Nuhu Pia yupo Juuko Murshid anayechezea timu ya Taifa ya Uganda ‘The Cranes’ ambayo leo inacheza nusu fainali.
“Kambi yetu hapa Zanzibar imeanza kupendeza baada ya wachezaji baadhi waliokuwa Ethiopia kuripoti kambini, tunaamini kuanzia kesho (leo) wote watakuwa wameshafika kambini,” alisema kocha huyo. Kwa upande wake Mratibu wa Simba mjini Zanzibar, Abbas Suleiman alisema jana kuwa timu yake leo itacheza na Kimbunga katika mchezo wa kirafiki Uwanja wa Amaan.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment