Wizara hiyo imesema kuwa mateka 900 wamekombolewa.
Operesheni hiyo ya siku tatu kuanzia Novemba tarehe 26- 28 kaskazini mwa nchi hiyo.
Idadi hiyo hata hivyo haijathibitishwa.
Huku hayo yakiarifiwa takriban watu tisa wameuawa katika mashambulio mawili ya kujitoa mhanga yaliyofanyika kwa wakati mmoja nchini humo.
Inashukiwa kuwa mashambulio hayo yamefanywa na wanamgambo wa Boko Haram .
Washambuliaji wawili walijilipua katika eneo la Waza Kaskazini mwa nchi karibu na mpaka wa Nigeria.
Wapiganaji wa Boko Haram wameimarisha harakati zao katika maeneo ya mipaka nchini Cameroon, Niger na Chad.
Cameroon ni miongoni mwa nchi zinazoshiriki juhudi za kieneo kukabiliana na wanamgambo hao.
0 comments:
Post a Comment