Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu
Hassan leo ameshiriki katika zoezi la kufanya usafi katika maeneo ya
Mtaa wa Oysterbay na Morocco stand katika wilaya ya Kinondoni katika
kuadhmisha miaka 54 ya uhuru wa Tanzania Bara.
Akizungumza na wananchi waliojumika katika maeneo ya Morroco stand
Makamu wa Rais amewaagiza viongozi wa wilaya za mkoa wa Dar es salaam
kutoa taarifa za wazabuni wa kufanya usafi ili ziweze kufuatiliwa.
“Haya makampuni yanapewa fedha kwa ajili ya kazi ya kufanya usafi;
lakini inaonyesha hayafanyi kazi ipasavyo kwa sababu mji bado ni
mchafu,” Alisema Mhe. Samia.
Alielezea kufurahishwa kwake kwa jinsi wananchi walivyojitokeza
katika zoezi hilo ambalo alisema ni endelevu na kuwataka Wakuu wa wilaya
na wenyeviti wa serikali za mitaa kupanga siku maalum kwa ajili ya
kufanya usafi katika maeneo yao.
Makamu wa Rais alisema Watanzania hawawezi kujivunia miaka 54 ya
uhuru ikiwa miji ni michafu na kuwataka wananchi kushirikiana kutekeleza
kauli mbiu ya uhuru na kazi kwa kila mmoja kufanya kazi bidii mahali
alipo aweze kuongeza tija ambayo italiwezesha Taifa kupata madawa na
elimu bora.
Pamoja na wananchi waliojumuika na Makamu wa Rais kufanya usafi
katika Mtaa wa Oysterbay, kwa upande wa Morocco stand walikuwepo pia
wafanyakazi wa benki ya DTB, Radio ya EFM na wasanii mbalimbali
0 comments:
Post a Comment