Image
Image

Wakulima wa Korosho wafaniki kulipwa bilioni 12 na MAMCU.

Baadhi ya vyama vya ushirika wa zao la korosho Mkoani Mtwara kikiwemo Chama Kikuu cha Ushirika cha Masasi na Mtwara  MAMCU, vimefanikiwa kuwalipa wakulima  kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 12.
Hiyo ni kwa ajili ya malipo ya kwanza na ya pili na bonasi kwa kipindi hiki cha ununizi wa korosho ukiendelea na kufuatia mafanikio hayo wakulima wameshauriwa kuacha kuuza korosho nje ya mfumo wa stakabadhi ghalani ili waweze kunufaika na kuipatia pia serikali mapato
Changamoto hiyo imetolewa na Kaimu Meneja Mkuu wa MAMCU Bwana KELVIN RAJABU na Katibu Mkuu wa Chama cha Msingi cha Kilimanjaro Bwana SAIDI HAMISI.
Licha ya kuwapo kwa mavuno machache ya korosho msimu huu kutokana na mvua chache ushindani wa minada ni mkubwa na wakulima wameweza kulipwa vizuri ukilinganisha na msimu wa mwaka jana.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment