Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John
Pombe Magufuli amefanya uteuzi wa wakuu wa Mikoa 26 ya Tanzania Bara, ambapo
kati yao 13 ni wapya, 7 wamebakizwa katika vituo vyao vya kazi, 5 wamehamishwa
vituo vya kazi na 1 amepangiwa Mkoa Mpya wa Songwe.
Uteuzi huo umetangazwa na Kaimu Katibu Mkuu
Kiongozi, Mhandisi Mussa Ibrahim Iyombe leo tarehe 13 Machi, 2016 Ikulu Jijini
Dar es salaam.
Wakuu wa Mikoa walioteuliwa ni kama ifuatavyo;
1. Mh. Paul Makonda - Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam.
2. Meja Jenerali Mstaafu Ezekiel Elias Kyunga - Mkuu
wa Mkoa wa Geita.
3. Meja Jenerali Mstaafu Salum Mustafa Kijuu - Mkuu
wa Mkoa wa Kagera.
4. Meja Jenerali Mstaafu Raphael Muhuga - Mkuu wa
Mkoa wa Katavi.
5. Brigedia Jeneral Mstaafu Emmanuel Maganga - Mkuu
wa Mkoa wa Kigoma.
6. Mh. Godfrey Zambi - Mkuu wa Mkoa wa Lindi.
7. Dkt. Steven Kebwe - Mkuu wa Mkoa wa Morogoro.
8. Kamishna Mstaafu wa Polisi Zerote Steven - Mkuu
wa Mkoa wa Rukwa.
9. Mh. Anna Malecela Kilango - Mkuu wa Mkoa wa
Shinyanga.
10. Mhandisi Methew Mtigumwe - Mkuu wa Mkoa wa
Singida.
11. Mh. Antony Mataka - Mkuu wa Mkoa wa Simiyu.
12. Mh. Aggrey Mwanri - Mkuu wa Mkoa wa Tabora.
13. Mh. Martine Shigela - Mkuu wa Mkoa wa Tanga.
14. Mh. Jordan Mungire Rugimbana - Mkuu wa Mkoa
Dodoma.
15. Mh. Said Meck Sadick - Mkuu wa Mkoa Kilimanjaro.
16. Mh. Magesa Mulongo - Mkuu wa Mkoa Mara.
17. Mh. Amos Gabriel Makalla - Mkuu wa Mkoa Mbeya.
18. Mh. John Vianey Mongella - Mkuu wa Mkoa Mwanza.
19. Mh. Daudi Felix Ntibenda - Mkuu wa Mkoa wa
Arusha.
20. Mh. Amina Juma Masenza - Mkuu wa Mkoa wa Iringa.
21. Mh. Joel Nkaya Bendera - Mkuu wa Mkoa wa
Manyara.
22. Mh. Halima Omary Dendegu - Mkuu wa Mkoa wa Mtwara.
23. Dkt. Rehema Nchimbi - Mkuu wa Mkoa wa Njombe.
24. Mhandisi Evarist Ndikilo - Mkuu wa Mkoa wa
Pwani.
25. Mh. Said Thabit Mwambungu - Mkuu wa Mkoa Ruvuma.
26. Luteni Mstaafu Chiku Galawa - Mkuu wa Mkoa wa
Songwe (Mkoa mpya).
Wakuu wote wa Mikoa walioteuliwa, wataapishwa
Jumanne tarehe 15 Machi, 2016 saa 3:30 Asubuhi Ikulu, Jijini Dar es salaam.
Gerson Msigw
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU
Dar es salaam
13 Machi, 2016


0 comments:
Post a Comment