Image
Image

TDA yazindua wiki ya afya ya kinywa na meno Kitaifa Dar es Salaam.

Serikali imewahakikishia watumishi wote katika sekta ya Afya kuwa imejipanga kuhakikisha inashughulikia changamoto zote zinazowakabili ndani ya sekta ya Afya huku ikiwataka kufanya kazi kulingana na matakwa ya viapo walivyoapa kwa ajili ya kuwahudumia wananchi.
Kauli hiyo imetolewa jijini Dar es Salaam na Naibu Waziri wa Afya Dkt Khamis Kigwangala,ambapo licha ya kuahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa chama cha madaktari wa kinywa na meno TDA, amewataka wataala hao kuzidi kutoa elimu ya kutosha kwa jamii kuhusu magonjwa ya kinywa na meno, huku akiwataka watalaamu wote kuhakikisha wanalinda misingi ya taaluma zao.
Katika hutuba ya rais wa chama cha madaktari wa afya ya kinywa na meno TDA,Dkt Lorna Carneiro amebainisha kuwa miongoni mwa shughuli zitakazofanyika kuelekea kilele cha maadhimisho hayo mach 20 mwaka huu mkoa morogoro ni pamoja na utoaji wa elimu ya kinywa na meno katika shule za mahitaji maalum zikiwemo za mtoni maalum, Sinza Maalum,Buguruni Maalum.
Watalaam wa afya ya kinywa na meno wanasema zaidi ya asilimia 30 ya watoto wenye miaka 12 wanakabiliwa na tatizo la meno kutoboka, huku asilimia 50 ya watoto wenye umri wa kubadilisha meno nao wakikabiliwa na changamoto hiyo.
Awali uzinduzi huo wa wiki ya kitaifa ya afya ya kinywa na meno ulitanguliwa na matembezi yaliyoongozwa na naibu huyo waziri wa afya, maendeleo ya jamii, wazee na watoto na kuhudhuliwa na madakatari na wadau mbalimbali wa afya ya kinywa na meno.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment