Image
Image

Ajali ya Saibaba na Canter yaua watatu arusha na kujeruhi.




Watu watatu wamefariki dunia na sita kujeruhiwa kwenye ajali iliyo husisha basi la saibaba lenya namba za usajili T720 ADE  na lori la mizigo aina ya Mitsubishi CANTER T 742 CRS  zilizo gongana uso kwa uso katika eneo la sakina jijini arusha.
Mashuhuda wa ajali hiyo wamesema kuwa tukio limetokea majira ya saa tisa usiku wa leo  wakati basi la saibaba likiwa kwenye majaribio kutoka arusha kuelekea ngara mtoni na lori likiwa linatokea oldonyo sambu kwenda arusha likiwa limebeba karoti ndipo basi linalodaiwa kuwa mwendo kasi likapanda tuta  kisha taa zikazimika na kupoteza mwelekeo na kugongana uso kwa uso.
Akizungumza kwa njia ya simu kamanda wa polisi mkoa wa Arusha liberatus Sabas amethibisha kutokea kwa ajali hiyo na kwataja waliyo fariki na kuwa dereva wa basi athumani saidck anashikiliwa na jeshi la polisi.
Wakati huo huo jitihada za kuokoa miili ya watu waliyo fukiwa na kifusi kwenye mgodi ya tanzatine one mererani zinaendelea na mwili mmoja wa mtu aliye fariki dunia aliyejulikana kwa jina la saidi mgosi umepatika huku waokoaji wakieleza hali ngumu iliyopo chini ya mgodo na mchimbaji aliyenusurika  gidesh benedict akakiri kumtambua na kueleza ilivyo kuwa.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment