Image
Image

Maafisa wakala 3 wa misitu watumbuliwa kwa udanganyifu wa uvunaji mazao ya Misitu Kasulu.


Serikali wilayani Kasulu kupitia kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo imewasimamisha kazi na kuwakamata maafisa watatu wa wakala wa misitu Tanzania TFS katika wilaya hiyo kutokana na kubainika kufanya udanganyifu katika uvunaji wa mazao ya misitu wilayani humo baada ya kukamata zaidi ya mbao elfu moja zikiwa zimevunwa kinyume cha sheria.
Akizungumza baada ya ukaguzi wa ghfla uliofanywa katika kijiji cha Mvugwe na kukamata mbao hizo, mwenyekiti wa kamati hiyo ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya Kasulu Gerald Guninita amewataja maafisa hao kuwa ni meneja wa wakala wa misitu wilaya ya Kasulu Donald Slaa na wafanyakazi wawili wa TFS William Skoi na Jonathan Kaiza ambao wamebainika kuhalalisha kwa kugonga muhuri wa serikali kwenye baadhi ya mbao nyumbani kwa mfanyabishara badala ya kufanya kazi hiyo porini na kwamba maafisa hao wamekuwa tatizo badala ya kuwa suluhisho la kulinda misitu katika wilaya hiyo.
Kwa upande wao wafanyabishara wa mbao katika kijiji cha Mvugwe wilayani Kasulu,wamelalamikia hatua ya serikali kukamata mbao zao, kwa kuwa wao wana vibali vyote vinavyowawezesha kuvuna mbao na kusafirisha. 

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment