Image
Image

Mwanamke asafiri na ndege akiwa kamficha mtoto kwenye begi.

Mwanamke mmoja alisafiri kwa ndege kutoka Istanbul nchini Uturuki hadi mjini Paris akiwa na mtoto aliyemficha katika begi lake la mkononi,shirika la ndege la Air Ufaransa limesema.
Shirika hilo limesema kuwa mtoto huyo aliyesafiri bila kulipa nauli alipatikana ndani ya ndege hiyo siku ya Jumatatu usiku.
Duru katika shirika hilo iliambia shirika la habari la AFP kwamba mwanamke huyo ni mkaazi wa Ufaransa ambaye alikuwa katika harakati za kumfanya mtoto huyo kutoka Haiti kuwa wake.
Shirika hilo la ndege lilielezea mamlaka ya Ufaransa lakini waendesha mashtaka wakaamua kutofungua mashtaka.
Mwanamke huyo alikuwa akingoja kuchukua ndege nyengine mjini Istanbul lakini akazuiliwa kupanda ndege hiyo na mtoto huyo ,duru hiyo iliarifu AFP.
Alinunua tiketi nyengine na kumficha mtoto huyo ndani ya begi.
Alipokuwa ndani ya ndege hiyo ,alimuweka mtoto huyo katika miguu na kujifunika na blanketi ,lakini mtoto huyo wa kike alitaka kwenda chooni na alionekana na abiria wengine.
Haijulikani mtoto huyo alikuwa na miaka mingapi ,duru moja ilieleza kwamba alikuwa na miaka minne huku nyengine ikisema alikuwa na mwka mmoja ama miwili.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment