Image
Image

Maghembe atumbua watumishi 6 wa sekta ya utalii kwa kusababishia serikali hasara ya bilioni 500.


Serikli imewasimamisha kazi watumishi sita wa sekta ya mistu akiwemo meneja wa kanda ya nyanda za juu kusini wa wakala wa huduma za misitu nchini TFS na mshauri wa maliasili wa mkoa wa Rukwa kwa tuhuma za kuzembea usimamizi wa misitu na kuisababishia serikali hasara ya zaidi ya shilingi bilioni 500.
Hatua hiyo imechukuliwa na waziri wa maliasili na utalii Profesa Jumanne Maghembe baada ya kufanya ziara ya kushitukiza katika mistu ya hifadhi ya wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa na kukuta magogo mengi yeneye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 500 yakiwemo yaliyokamatwa na vyombo vya dola na mengine yakiwa bado msituni katika harakati za kuyasafirisha kwenda nje ya nchi na ameagiza yakusanywe yote na serikali itafanya mchakato wa kuyapiga mnada na fedha zitakazopatikana zitumike kwa manufaa ya uma.
Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Kalambo Wilman Ndile amesema kwa muda mrefu kumekuwa na baadhi ya watumishi wasio waaminifu ambao wamekuwa wakishirikiana na wahalifu kuvuna msitu katika wilaya hiyo kinyume cha sheria na kuyapeleka upande wa Zambia kupata vibali bandia vinavyoonyesha kuwa magogo hayo yamevunwa upande wa zambia hali ambayo imesababisha uharibifu mkubwa wa misitu ya wilaya ya kalambo.
Nae mkurugenzi wa wakala wa huduma za misitu nchini TFS,Juma Mgoo amesema serikali itaongeza nguvu katika kusimamia misitu ikiwemo kuajiri watumishi wapya na walinzi wa misitu ili kuokoa rasilimali za taifa zinazoteketea na kusababisha uharibifu mkubwa wa misitu ikiwemo ya vyanzo vya maji.
Watumishi waliosimamishwa wametajwa kuwa ni pamoja na meneja wa nyanda za juu kusini wa wakala wa huduma za misitu nchini tfs, mshauri wa maliasili mkoa wa rukwa, na mameneja wa TFS wa wilaya za Kalambo na sumbawanga pamoja na maafisa misitu wa halmashauri za wilaya za kalambo na sumbawanga mkoani Rukwa.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment