Image
Image

Polisi yathibitisha vifo vya watu 4 akiwemo dereva wa daladala na majeruhi 26 Tabata Matumbi jijini Dar es Salaam.


Watu wanne wamekufa papo hapo na wengine 26 wamejuriwa katika ajali ya gari iliyohusisha magari matatu iliyotokea  katika barabara ya mandela eneo la kwa Ali Hamza jiji Dar es Salaam.
Kamanda wa polisi kandaa maalumu ya Dar es Salaam,Kamishna Simon Sirro amesema tukio hilo limetokea majira ya saa 11 alfajiri ambao dereva lori ya mchanga lenye namba za usajili T44 DBH 7 likielekea Ubungo aliigonga nyuma daladala Toyota DCM yenye namba za usajili T629 CRT na kusababisha ipoteze mwelekeo na kuhamia upande wa pili wa barabara ambapo ikagongana na lori aina SCANIA yenye namba za usajili T109 DDX lililokuwa limebeba Ngo'ombe na kusabaisha vifo vya abiria watatu na dereva wa daladala hapohapo.

Kufuatia ajari hiyo baadhi ya majeruhi walikuwa katika hali mbaya wameamishiwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili,ambapo akizunguza na waandishi wa habari afisa uhusiano wa Hospitali hiyo,Bi  Neema Mwangamo amekiri kupokea majeruhi watano ambao wako katika chumba cha uangalizi maalum na wengine wameamishiwa katika taasisi ya tiba ya Mifupa-Moi- kwa matibabu zaidi.
Aidha akizungumza na waandishi wa habari meneja ustawi wa jamii na Mahusiano wa taasisi ya tiba mifupa-moi- Bwana Juma Almasi amesema jumla ya majeruhi sita wamefikishwa katika taasisi hiyo kutoka hopsitali ya taifa ya muhimbili idadi kubwa wakiwa wameumia katika sehemu za miguu na vichwani na kuisisitiza wote wametambilika majina na maeneo wanayoishi.
Idadi kubwa ya majeruhi wa ajali hiyo wamelazwa katika hospitali ya amana iliyopo manispaa ya ilala.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment