Image
Image

Ramos awataka waliomzomea cristiano ronaldo kujitafakari.


Beki mkongwe wa real madrid Sergio Ramos amesema mashabiki wa timu hiyo waliomzomea cristiano ronaldo kwenye mechi ya jana usiku dhidi ya ligi ya mabingwa ulaya dhidi ya as roma wanatakiwa kufikiri kwanza.
Ronaldo alifunga bao moja na kutoa pasi ya mwisho kwenye goli la pili la mchezo huo ambapo real ilishinda mabao 2 kwa bila na kujihakikishia nafasi kwenye roo fainali ya ligi ya mabingwa ulaya msimu huu.
Mreno huyo alizomewa na baadhi ya mashabiki wa real madrid kwenye mechi hiyo kitenfo hicho kikihusishwa na kauli yake ya mwezi febrauri kuwa wachezaji wenzake hawana uwezo kama wa kwake na ndo mana timu yao lilifungwa na atletico madrid bao 1 kwa bila.

Sergio ramos ambaye ndo kapteni wa timu hiyo amesema mashabiki wanatikuwa kufikiria kabla hawajamzomea mchezaji huyo kwani anamchango mkubwa kwneye timu hiyo.
Kwa upande wake kocha wa real zinedine zidane amesema walomzomea ronaldo wamemuongezea tu hamsa ya kufanya vyema kwenye michezo inayofuata.
Nchini uingereza jinamizi la manchester united limeanza kuiandama arsenal na kocha wake arsene wenger tayari ameshaanza kuonesha wasiwasi wake kutokana na kuumia kwa wachezaji wake muhimu kwemye mechi ya pili ya kombe la fa ambapo timu hiyo ilishinda mabao 4 kwa 0 dhidi ya hul city.
Kiungo wa timu hiyo aaron ramsey alitolewa nje dakika 16 baada ya kuingia kama mchezaji wa zida kwenye kipindi cha pili na kuumia.
Walinzi per mertesacker and gabriel nao wameongeza tatizo la majeruhi hasa upande wa mabeki huku laurent koscielny akiwa bado hajapona.
Arsenal walishinda mechi hiyo ya pili ya mzunguko wa 5 wa fa cup na sasa watacheza robo fainali dhidi ya watford jumapili.
Na ushindi wa wikiendi hdidi ya warriros umeonekana kuwatia nguvu los angeles lakers ambao alfajiri ya leo wamewafunga orlanod magic kwa alama 107 kwa 98.
D'angelo russell aliendlea kuwafirahisha mashabiki wa staples centre kwa namna alivyokuwa akicheza na kufanikiwa kutumbukiza alama 27.
Julius randle aliongeza vingine 23 huku jordan clarkson akifunga 24 na kuwamaliza kabisa magic ambao alfajiri ya jana walifungwa na warriors.
Mpaka mechi hiyo inaanza lakers bado walikuwa wakishikilia rekodi ya timu mbovu ya pili kwenye msimu baada ya kufungwa mechi 51 wakishinda 14 tu.
Rekodi hiyo inashikiliwa na phoeniz suns.



Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment