Image
Image

Mkwasa kushirikiana na kamati ya ufundi kuipa mbinu Twiga Stars mchezo wa marudio na Zimbabwe.


Kocha mkuu wa taifa Stars Charles Boniface Mkwassa amejitolea kushirikiana na benchi la ufundi la timu ya taifa ya wanawake Twiga Stars kukiandaa kikosi cha timu hiyo kwa ajili ya mchezo wa marudiano dhidi ya Zimbabwe wa kusaka tiketi ya kushiriki fainali za Afrika ambazo zimepangwa kufanyika nchini CAMEROON mwishoni mwa mwaka huu.
Mkwassa ambaye kabla ya kupewa kibarua cha kukinoa kikosi cha taifa Stars aliwahi kuwa kocha mwenye mafanikio wa Twiga Stars ambaye aliiwezesha timu hiyo kufuzu kwa fainali za Afrika za wanawake mwaka 2010 zilizofanyika nchini afrika kusini amesema alikwepo uwanjani wakati Twiga Stars ilipochezea kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Zimbabwe mwishoni mwa wiki iliyopita na kubaini mapungufu ambayo ameona anaweza kusaidia kuelekea mchezo wa marudiano.
Kocha huyo maarufu kwa jina la 'MASTER' kutokana na umahiri aliokua nao wa kusakata kandanda enzi zake amesema ameguswa na matokeo waliyopata twiga Stars hivyo amejitolea kushirikiana na benchi la ufundi la timu hiyo chini ya kocha nasra juma kuangalia makosa ya kiufundi na kuyarekebisha kabla ya kukwea pipa kwenda zimbabwe kwa ajili ya mchezo wa marudiano.


Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment