Image
Image

Msongamano Hosipitali ya KCMC watishia usalama wa wagonjwa.




Msongamano mkubwa wa wagonjwa katika Hospitali ya rufaa ya KCMC umesababisha madaktari kutoa huduma katika mazingira  magumu na hatari kwao wenyewe na pia kwa wagonjwa na serikali  imeombwa kuongeza jitihada za kuboresha hospitali za mikoa  na wilaya ili kupunguza tatizo hilo .
Idadi  kubwa  ya  wagonjwa wameonekana wakiwa wamelazwa  nje  ya  wodi na  kwenye  njia  za  kuingia  wodini  hali  ambayo mkurugenzi mtendaji  wa  Hosipitali hiyo amesema wanaendelea kuikabili  kwa  kuongeza  majengo  likiwemo  la tiba ya moyo  linalojengwa  kwa  ufadhili  wa  Mwenyekiti  mtendaji wa  makampuni  ya  IPP  Dr.Regnald Mengi.
Hata hivyo  baadhi  ya  wagonjwa  wamesema  licha  ya kulazwa  knje ya  wodi  meendelea  kuhudumiwa    na wameandikiwa  kuja  katika    hosipitali hiyo  kutokana  na   ukosefu  wa  huduma  bora , madaktari  wenye  sifa  na vitendea  kazi katika  hosipitali  za miko , wilaya  na  vituo  vya  afya.
Baadhi ya    wasimamizi   na  wadhamini   wa  hosipitali hiyo   iliyoanzishwa  miaka  45  iliyopita  ikiendeshwa  kwa  ushirikiano  wa  serikali  na  kanisa  la  kkkt   ambayo  inahudumia  wagonjwa  kati  ya  600  na  800  kwa  siku  ikiwa  na   vitanda  600  wamewataka  watendaji  kuongeza  uwajibikaji  ili  kukidhi  matarajio  ya  wogonjwa  na  kuendelea  kuwapa  moyo  na  imani.
Kcmc  ni miongoni mwa  hosipitali  nne  kubwa  za  rufaa  hapa  nchini  ambazo  zimekuwa kimbilio la  wananchi wenye  magonjwa  yaliyoshindikana  maeneo  mengine,nyingine  ikiwa  ni  muhimbili , iliyoko  daressalam , bugando  ya  mwanza na hosipitali  ya rufaa  ya  mbyeya.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment