Image
Image

Polisi waimarisha ulinzi baada ya wafuasi wa CHADEMA kufurika Mahakama kuu Mwanza.


Jeshi la polisi jijini Mwanza limelazimika kuimarisha ulinzi wa hali ya juu baada ya wafuasi wa CHADEMA kufurika katika Mahakama kuu jijini Mwanza wakifuatilia kesi ya ubunge ya aliyekuwa Mbunge wa Nyamagana Ezekiel Wenje.
Inaelezwa kuwa shughuli mbalimbali za kijamii na uchumi zilisimama kwa muda wa saa mbili kufuatia wingi wa wafuasi wa CHADEMA kuwepo Mahakamani hapo.
Kesi hiyo ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu 2015 kati ya aliyekuwa  Mbunge wa zamani Ezekia Wenje jimbo la Nyamagana na Mbunge wa sasa Stanslaus Mabula kesi hiyo ilisimamishwa kuanzia saa 6 mpaka 8, ndipo mahakama iendelee kusikiliza mashahidi wa upande wa Wenje.
Tutaendelea kukufahamisha kinachoendelea,Toa maoni yako hapo Chini.



Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment