Image
Image

Serikali kuongeza ushiriki wa wanawake katika ngazi za Kimamuuzi.



Serikali imesema katika kuhakikisha usawa wa kijinsia unapatikana nchini vipo baadhi ya vipaumbele ambavyo imewiweka ili kufikia usawa huo ikiwemo kuongeza ushiriki wa wanawake katika ngazi za kimamuuzi pia kusimamia upatikanaji wa haki na sheria kwenye masuala yanayowakumba wanawake.
Hayo yamesemwa na waziri wa nchi,Ofisi ya Rais-Utumishi na Utawala bora Mh.Angella Kairuki alipokuwa akizindua kampeni iliyoshirikisha wanawake toka maeneo mbalimbali ya jiji la Dar es Salaam yenye lengo la kumsaidia Mwanamke ya namna anyoweza kujikomboa kifikra na kiuchumu iliyoandaliwa na taasisi ya haki za wanawake ambapo amesema serikali inatambua changamoto zinazowakabiri wakina mama wa kitanzania na hivyo itashirikiana nao kuhakikisha zinapatiwa ufumbuzi.
Kampeni hiyo yenye kauli mbiu isemayo 'Mwanamke Piga Kazi usikubali Mapenzi yakatishe ndoto zako ambapo moja kati ya mwanaharakati wa masuala ya wanawake amewataka wanawake kuacha dhana ya kuwa tegemezi na kupiga kazi ili kujikomboa kiuchumi.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment