Mwenyekiti wa chama cha Demokrasia na Maendeleo
CHADEMA Mh.Freeman Mbowe,amesema migogoro
ndani ya chama hicho iliyosababishwa na Rushwa, utovu wa nidhamu na
maadili kwa baadhi ya viongozi wake wa ngazi mbalimbali,ndiyo sababu kubwa
iliyokifanya kupoteza ushindi wakati wa uchaguzi mkuu uliopita.
Kauli hiyo imetolewa na Mh.Mbowe wakati akifungua
kikao cha baraza kuu la chama hicho jijini mwanza, kinachohudhuriwa na wajumbe
zaidi ya mia tano, mwenyekiti huyo wa chadema taifa ambaye pia ni mbunge wa
jimbo la hai mkoani kilimanjaro, amesema kamati kuu inapendekeza kwa baraza kuu
kuundwa kwa kamati ya maadili kitaifa ambayo itakuwa chini ya makamu mwenyekiti
wa chadema taifa, prof. Abdallah safari.
Mh. Mbowe ambaye pia ni kiongozi wa kambi rasmi ya
upinzani bungeni ametumia fursa hiyo kukanusha propaganda zinazoenezwa na
mahasimu wao kisiasa kwamba, aliuza chama hicho kwa aliyekuwa mgombea urais wa
chadema akiungwa mkono na vyama vinavyounda umoja wa katiba ya wananchi (UKAWA
) Mh. Edward Lowassa.
Kwa upande wake, aliyekuwa mgombea urais wa chama
hicho katika uchaguzi mkuu wa oktoba 25 mwaka jana Mh.Edward lowassa,
amewashukuru wananchi kwa kujitokeza kwa wingi kumpigia kura, wakiwemo wale
waliomfuata na kumuomba kutoa tamko kuhusu msimamo wake baada ya mwenyekiti wa
tume ya taifa ya uchaguzi jaji mstaafu damian lubuva kutangaza matokeo ya urais.
0 comments:
Post a Comment