Image
Image

Uamuzi wa Ghana kurahisisha utaratibu wa visa kwa wanachama wa Umoja wa Afrika wakaribishwa.

Mwenyekiti wa kamati ya Umoja wa Afrika Bibi Nkosozana Dlamini Zuma amekaribisha uamuzi wa Ghana wa kutoa visa kwa watu kutoka nchi wanachama wa Umoja wa Afrika wakati wanafika Ghana.
Rais John Dramani Mahama wa Ghana alitangaza uamuzi huo wakati akilihutibia bunge Februari 25. Alisema kuanzia mwezi Julai mwaka huu, Ghana itawaruhusu watu kutoka nchi zote wanachama wa Umoja wa Afrika kuingia Ghana na kupewa visa ya muda wa siku 30, uamuzi aliosema utahimiza usafiri wa ndege, biashara, uwekezaji na utalii.
Bibi Zuma amepongeza uamuzi wa Ghana uliopitishwa na baraza la utendaji la Umoja wa Afrika mwanzoni mwa mwaka huu. Bibi Zuma amesema anatarajia kuwa nchi nyingine za Afrika zitafuata hatua ya Ghana, ili kuhimiza mafungamano, maendeleo na amani barani Afrika.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment