Image
Image

Baada ya Magufuli kumtumbua Kilango wachambuzi wazungumza haya hapa.


Baadhi ya wanasiasa wakongwe pamoja na wachambuzi mbalimbali waliozungumza na mtanzania, walieleza kusikitishwa na uamuzi  wa rais magufuli, wakisema ni wa kukurupa huku wengine wakipongeza hatua hiyo.
Sumaye.
waziri mkuu mstaafu, frederick sumaye alisema kilango hakuwa na hatia kiasi hicho kwa sababu bado hajaujua vizuri mkoa huo.
“ukweli haiwezekani rc asimamie jambo hilo muda mfupi na hata akipewa miezi sita akakague watu hao ‘physically’ bado haitoshi.
“kama aliletewa taarifa kuwa kuna watumishi hewa na yeye akasema hakuna…hapo kuna tatizo. lakini ndio hivyo kila mtu na utawala wake, kumwajibisha mtu ambaye hata huo mkoa na ofisi hajaijua vizuri kwa kweli inasikitisha. hii haijapata kutokea popote na si kitu cha kawaida,”alisema sumaye.
Prof baregu.
kwa upande wake, mjumbe wa kamati kuu ya chama cha demokrasia na maendeleo (chadema), profesa mwesiga baregu alisema kuna udhaifu mkubwa wa namna ya kuwapata wakuu wa mikoa, wilaya na makatibu wakuu.
profesa baregu aliyepata kuwa mjumbe wa iliyokuwa tume ya mabadiliko ya katiba, alisema nafasi hizo zimekuwa zikitolewa kisiasa na ndio maana kumekuwapo na matatizo ya mara kwa mara kwa sababu viongozi hao hawajachekechwa.
“hizi nafasi zilipaswa zipatikane kwa usaili yaani watu waombe au wapendekezwe halafu ndio wapewe nafasi hizo, lakini nafasi hizo zimekuwa zikitolewa kisiasa ndio maana haya yote yanatokea,”alisema msomi huyo.
alisema kosa la pili alilolifanya rais magufuli, ni namna alivyotoa maagizo wakati kuna vyombo na taasisi zinazohusika katika uchunguzi, badala ya wakuu wa mikoa ambao hawana utaalamu wowote.
“kwanini hakutaka kutumia vyombo vya ukaguzi na badala yake anawaambia wakuu wa mikoa? tuna ofisi ya cag na pale kuna watumishi wengi wa ukaguzi wangeenda wilayani na mikoani kufanya uchunguzi lakini kuwaachia marc ambao wengine ni walewale waliokuwepo katika baadhi ya mikoa…yaani ajikague mwenyewe halafu akuletee?
“rc hajui jinsi ya kuhesabu…katika hili rais magufuli amekurupuka kwa sababu kazi hiyo ilipaswa kufanywa na vyombo husika viandae taarifa kitaalamu. sasa kwa sababu na yeye kilango alipewa nafasi hii kisiasa naye anakubali na hana namna.
“bado kazi ya ukaguzi kwa watumishi hewa haijafanyika ipasavyo, mpaka likifanyika kitaalamu ndio tutaelewa kwa sababu wapo ambao si hewa lakini wameunganishwa,”alisema profesa baregu.
Wasira.
 mwanasiasa mkongwe aliyepata kushika nyadhifa mbalimbali serikalini, steven wasira alisema alichokifanya rais magufuli ni kawaida kwa sababu kila kiongozi ana aina yake ya uongozi.
“lakini hata wakati wa nyerere (mwalimu julius) jambo kama hili lilitokea, kuna mtumishi mmoja simkumbuki kwa jina aliteuliwa na baadaye ikabainika hana sifa akatenguliwa ndani ya muda mfupi. lakini hili ni jambo la rais yeye ndiye ana mamlaka ya kuteua na kutengua,”alisema wasira.
Msekwa.
kwa upande wake, mwanasiasa mkongwe na spika mstaafu, pius msekwa alisema kila zama na kitabu chake na kwamba haiwezekani kuufananisha uongozi wa magufuli na viongozi waliopita.
“ni sahihi alichokifanya rais kwa sababu ndio ‘style’ yake ya uongozi na yeye ndio mwenye mamlaka ya kuteua na kutengua,”alisema.
Dk.Bisimba.
naye mkurugenzi mtendaji wa kituo cha sheria na haki za binadamu (lhrc), dk. hellen kijo bisimba alisema pamoja na kasi ya rais magufuli, lakini hajamtendea haki kilango kwa sababu bado alikuwa mgeni katika mkoa huo.
“huyu alikuwa ndio amefika tu na pengine watendaji ndio waliomdanganya sioni sababu ya yeye kuwajibishwa. angepewa hata onyo kuwa awe mwangalifu zaidi.
“na kwa mtazamo wa kijinsia tunaweza kudhani labda kwa sababu ni mwanamke kwani hata rais anaweza kupewa taarifa za uongo na watu wa chini yake, lakini hatutamtoa madarakani,”alisema dk. bisimba.
Prof. Mpangala.
mhadhiri wa chuo kikuu kishiriki cha ruaha (ruco), profesa gaundence mpangala alisema alichokifanya rais magufuli ni hatua za kinidhamu kwa watumishi wa serikali na kwamba wengine wajifunze.
    bana.
naye mhadhiri wa chuo kikuu cha dar es salaam (udsm), dk. benson bana alisema alichokifanya rais itakuwa fundisho kwa viongozi waliopewa dhamana.
Machali.
aliyekuwa mbunge wa kasulu mjini, moses machali, aliandika kupitia ukurasa wake wa facebook akimpongeza rais magufuli kwa hatua aliyoichukua.
“kiukweli,  salute kwako ‘mr president’ kama kweli inavyoripotiwa mitandaoni kwamba umetengua uteuzi wa mkuu wa mkoa wa shinyanga ambaye ni mteule wako, tena wa juzi juzi tu, si jambo jepesi kwa kiongozi kumwadabisha mteule wake hapa afrika na hasa tanzania.
“naanza kuiona tanzania mpya na kuamini uliyowaasa wateule wako mbalimbali, tukio hilo litaongeza umakini na kuwafanya wakuu wa mikoa na wateule wengine serikalini kujenga tabia ya kufuatilia au kufanya uchunguzi au utafiti wa masuala yanayopaswa kutekelezwa na wao… keep it up mr president,” alisema machali.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment