Image
Image

EAC yazitaka nchi mwanachama wa jumuia hiyo kuiga utatuzi wa migogoro kutoka Tanzania.

Jumuiya ya Afrika  Mashariki imezitaka nchi wanachama  wa jumuiya hiyo kuiga mfumo wa utatuzi wa migogoro unaotumiwa na Serikali ya Tanzania wa kutumia nguvu kubwa ya ushawishi,na mazungumzo kuondoa chochoko zinazoweza kusababisha  umwagaji wa damu usio wa lazima badala ya kusubiri kutumia nguvu  hizo madhara yakishatokea.
Changamoto hiyo im etolewa na Katibu Mkuu wa jumuiya hiyo,Dakta.RICHARD SEZ I BERA alipokuwa  akizungumza na makundi   mbalimbali ya wananchi na watendaji waliojitoka  kuwakumbuka Mamilioni ya wananchi waliopoteza ma isha katika mauaji ya  kimbari ya Rwanda mwaka 1994 .
Wakizungumza mwishoni mwa hafla hiyo washiriki kutoka nchi mbalimbali,wakiwemo walionusurika kwenye mauaji hayo ya  kimbari na mengine yanay osababishwa na masuala ya siasa katika nchi zao ambao walifanya maandamano na kuweka mashada  ya maua katika mnara ulioko kwenye Makao Makuu ya jumuiya hiyo wameishukuru Tanzania kwa kuwa kuwa jirani mwema na kimbilio  la wote wenye shida.
Kwa upande wake mwakilishi wa Serikali ya Tanzania katika hafla hiyo ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Arumeru,WILSON  NKAMBAKU amesema lengo la Tanzania ni kuona wananchi wa nchi zote wanaishi kwa amani.
.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment