Image
Image

Kapombe amekwishaanza matibabu Afrika Kusini.



Beki wa pembeni wa Azam FC Shomary Salum kapombe ameanza matibabu nchini Afrika kusini akiwa chini ya uongozi wa timu ya Bidvest ya nchini humo.
Msemaji wa Azam FC Jaffery Iddy Maganga amesema, Kapombe amepokelewa na uongozi wa Klabu ya Bidvest ambao walitengeneza ukaribu baina na timu hiyo bila kujali wala kuangalia kuwa walicheza na timu hiyo na kuitoa katika michuano ya kombe la Shirikisho Afrika.
Maganga amesema, Kapombe amefikishwa hospitali ya Morningside Mediclinic na ameanza kupatiwa matibabu baada ya kugundulika na ugonjwa wa Pulmonary Embolism ambao ni donge la damu kuziba mishipa ya damu katika mapafu.
Maganga amesema, Kapombe atakaa kwa takribani wiki mbili kwa ajili ya matibabu na baada ya kurejea nchini atakaa kwa takribani miezi miwili ili kujiangalia afya yake kabla ya kurudi mchezoni.
Maganga amesema, kukosekana kwa Kapombe kumekuwa ni pigo kwa upande wao kwani ni mchezaji ambaye alikuwa sababu ya timu kutumia mfumo ambao walikuwa wakiutumia na ndio maana katika mchezo dhidi ya Esperance ya Tunisia mwishoni mwa wiki iliyopita waliamua kubadili mfumo wa uchezaji.
Kapombe aliyekosa mechi mbili zilizopita za Azam FC dhidi ya Toto Africans na Ndanda, alianza kuumwa na kifua wakati kikosi hicho kikijiandaa kuvaana na Toto jijini Mwanza kabla ya kukimbizwa hospitalini.
Kapombe ataukosa mchezo wa marudiano dhidi ya Esperance utakaopigwa Aprili 19 nchini Tunisia pamoja na mechi zote za Ligi kuu ya soka Tanzania bara zilizobakia za Azam FC msimu huu na huenda akarejea uwanjani kwenye kipindi cha maandalizi ya msimu ujao.
Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment