Image
Image

Barcelona yavuliwa ubingwa baada ya kutandikwa bao 2-0 na Atletico Madrid.

Mabingwa watetezi wa Ligi ya Mabingwa Ulaya wametolewa katika michuano hiyo wakati magoli mawili ya Antoine Griezmann yakiibeba Atletico Madrid na kutinga katika nusu fainali za michuano hiyo.

Barcelona iliwasili katika Jiji la Madrid ikiwa na ushindi wa mabao 2-1 katika mchezo wa awali lakini uzembe wa mabeki wake ulimfanya Griezmann ambaye alikuwa hana mtu wa kumkaba kupachika bao la kwanza na kisha baadaye kupachika la pili kwa penati.

Katika mchezo mwingine Bayern Munich ilifanikiwa kutinga nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa kupambana na kiume na Benfica na kutoka sare ya mabao 2-2.

Timu hiyo ya Ureno iliyokuwa nyuma kwa bao 1-0 dhidi ya Bayern Munich katika mchezo wa awali, walijipa matumaini baada ya Raul Jimenez kupachika bao la kwanza katika mchezo wa jana.

Hata hivyo Arturo Vidal na Thomas Muller walifunga magoli na kuiweka klabu hiyo ya Ujerumani katika nafasi ya kusonga mbele licha ya Talisca kusawazisha na kufanya matokeo kuwa 2-2.

Share on Google Plus

Kuhusu TAMBARARE HALISI

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment